Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 106

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:20 PM

Page 91

katika Uislamu

ya nyota) mashuhuri na mwanahisabati pia, aliyeitwa Umar Khayyam wa huko Nishapur; India, (wakati William the Bastard akiiteka England), alikuwa amewapa Iran kalenda (Jalali Calendar) ambayo hadi hivi leo ndiyo inayotuwezesha kuanza mwaka mpya kwa usahihi wa saa, dakika na sekunde na siyo kwa kufuata siku tu! Hayo ni mahesabu aliyoyafanya mwanasayansi huyo enzi hizo zisizo na vifaa vya kisasa lakini kwa usahihi wa hali ya juu unaokamilisha mzunguko mmoja (orbit) kuzunguka jua. Mifano ya wanasayansi waliozuiwa na Kanisa kutoa uvumbuzi wao, ipo kadhaa wa kadhaa lakini nafasi haitoshi kueleza yote. Kwa upande wa nchi za kiislamu za wakati huo, mnamo miaka ya 794 A.D. chini ya utawala wa Bani Abbas, khalifa Ma’amun alizindua ‘Nyumba ya Maarifa’ huko Baghdad kama kituo cha sayansi. Aliweka humo vyombo vya uchunguzi wa anga, maktaba ya wazi (public library), ambapo alitumia Dinari 200,000 (dola million saba). Aliwakusanya hapo wasomi maarufu wajuzi wa lugha za nje na taaluma tofauti. Khalifa huyo alitenga pesa nyingi za kuwezesha kuwatuma nchi mbali mbali kukusanya vitabu juu ya sayansi, tiba, hekima, hisabati na ujuzi wa lugha mbali mbali. Wakusanyaji hao wa vitabu walituma huko mzigo wa vitabu uliobebwa na ngamia 100! Miaka hiyo Ulaya yote haikuwa na chuo kikuu hata kimoja. Katika kitabu chake kiitwacho: History of Islamic and Arab Civilisation, Dr. Gustave Le Bon anaandika, katika uk. 329, juzuu ya tatu, kwamba: “Siku hizo wakati vitabu na maktaba havikuwa na maana yoyote Ulaya, nchi nyingi za kiislamu zilikuwa na vitabu na maktaba kwa wingi. Huko Baghdad katika ‘Nyumba ya Maarifa’ kulikuwa na vitabu milioni nne; na huko Cairo katika Maktaba ya Mfalme, vitabu milioni moja, na huko katika maktaba ya Syria, vitabu milioni tatu. Huko Spain wakati wa utawala wa Waislamu, kulikuwa na uchapishaji (publication) wa vitabu kati ya elfu 70 hadi 80 kila mwaka.” Mnamo mwaka wa 1300 A.D. mwanzoni, bwana ‘G.L. Estrange katika kitabu chake: ‘The Legacy of Islam’ ukurasa 230 anaeleza kuwa ‘Chuo 91


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.